Habari kutoka kwa serikali ya Afghanistan zimeiambia BBC kuwa
kinara mkuu wa kundi la wapiganaji wa Taliban, Mullah Omar amefariki.
Lakini habari hizo bado hazijathibitishwa rasmi na kundi hilo , Kwa miezi kadhaa
kumekuwepo na tetesi kuhusiana na kifo cha Mullah Omar.
Kifo hicho kimetokea wakati ambapo serikali ya Afghanistan ilikuwa inajiandaa kuanza
mashauriano ya amani na kundi hilo
la Taliban.
Waandishi wa habari wameitwa na serikali ili kuhudhuria
kikao cha wanahabari jijini Kabul ,
ambao unatazamiwa kufanyika muda mchache ujao, Taarifa nyingine zinasema kuwa
huenda alifariki miaka kadhaa iliyopita.