Wanajamvi, kale kamchezo ka Mwigulu kujiona yupo juu ya
sheria na kutoa rushwa kila kona ya Iramba imemtokea puani baada ya kukamatwa
na kuhojiwa na Takukuru kwa muda wa zaidi ya masaa matatu.
Wagombea wenzake walijitoa katika kinyang'anyiro tangu
tarehe 25 kwa madai ya kufanyiwa rafu hizo na kutoa malalamiko yao
huku wakisubiri suala hilo
kushughulikiwa ndipo warejee kwenye kampeni.
Ofisi ya Takukuru mkoani Singida imemuhoji kwa masaa kadhaa
naibu waziri wa fedha na aliye kuwa mbunge wa Iramba Magharibi Mheshimiwa
Mwigulu Nchemba, kwa tuhuma za kukiuka sheria ya garama ya uchaguzi na sheria
ya kuzui na kupambana na rushwa.
Akiongea na waandishi wa habari mkuu wa Takukuru mkoani
Singida Bwana Joshua Msuya amesema Mheshimiwa Mwigulu Nchemba amekiuka sheria
ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11/2007 katika zoezi linalo ndelea la
kura za maoni ndini ya vyama vya siasa.
Katika hatua nyingine Bwana Msuya amewatahadharisha wagombea
wote wa ngaza mbalimbali watakae jihushisha na kutoa rushwa iwe ya fedha au
vitu,vifaa vya michezo, madawati watakuwa wamekiuka sheria ya kuzuia na
kupambana na rushwa namba 11/2007 na sheria ya uchaguzi cap.343 r.e 2002 na pia
sheria ya garama za uchaguzi namba 6/2010.
Katika jimbo la Singida kaskazini wa tia nia saba ambao
wanagombea ubunge kwa tiketi ya CCM, wametishia kujitoa katika kinyanganyiri
hicho kufuatia msimamizi wa uchaguzi kumwachia mgombea mwenzao ambaye ndiye
mbunge wa jimbo hilo
kuto kufuata masharati ya sheria za uchaguzi jambo ambalo limekuwa kero hadi
kutumia vijana wa shule kuonyesha vipeperushi vyake wakati wa mkutano wa
kujinadi.
ITV haikuishi hapa ilifanya juhudi za kumwona kaimu katibu
wa CCM mkoa wa Singida ambaye ndiye msimamizi mkuu wa mkoa Bwana Aluu Segamba,
amekiri kuwepo kwa matatizo hayo na kuchukuwa jukumu la kumbadilisha msimamizi
wa uchaguzi wa jimbo hilo na kumweka mwingine.
Baadhi ya majimbo ya uchaguzi yenye wabunge ambao wameamua
kutia nia ya kugombea tena wamekuwa wakioneka wao ni chanzo kimoja wapo kikubwa
cha kuvunja mashariti ya uchaguzi na kuwasababishia wenzao kuwa na malalamiko
mengi,hadi kufikia hatua ya kuiomba serekali kupeleka maafisa wa takukuru na
polisi kwenye mikutano ya kujinadi kugombea ubunge.