Katika hotuba ya kwanza ya rais wa Marekani kwa muungano wa
Afrika katika makao makuu ya umoja huo mjini Addis Ababa ,amesema kuwa Afrika haitapiga hatua
iwapo viongozi wake watakataa kuondoka madarakani baada ya muda wao kuisha.
Amemtaja hayati Nelson Mandela wa Afrika Kusini, ambaye
alikaa madarakani kwa muhula mmoja tu wa miaka mitano na anafahamika pakubwa
kote duniani huku akiheshimiwa kama kigogo wa
bara Afrika, tofauti na marais wengi wanaoendelea kukwamia madaraka.
Ameongezea kuwa wakati waandishi wanapofungwa huku
wanaharakati wakitishwa,demokrasia huwepo tu kwa jina, Akimnukuu shujaa Nelson
Mandela akisema kuwa unapoheshimu uhuru wa wengine watu wote huwa huru.
Amesema kuwa ishara kuu ya maendeleo katika taifa ni vile
linavyowachukulia wanawake wake.
Amewaambia viongozi wa Afrika kwamba maendeleo ya bara hili
yanategemea demokrasia,uhuru na haki za kibinaadamu, Anasema kuwa muda umewadia
wa kubadilisha mtizamo wa Afrika kama bara duni lenye kulemewa na umaskini na
mizozo.
Aidha amepongeza umoja wa Afrika AU na shirika la Umoja wa
mataifa katika mapambano dhidi ya makundi ya wapiganaji wa kiislamu kama vile,
Boko Haram kaskazini mwa Nigeria
na Al - Shaabab Afrika mashariki.
Amemtaja hayati Nelson Mandela wa Afrika Kusini, ambaye
alikaa madarakani kwa muhula mmoja tu wa miaka mitano na nafahamika pakubwa
kote duniani huku akiheshimiwa kama kigogo wa
bara Afrika, tofauti na marais wengi wanaoendelea kukwamia madaraka.