Raia wa kigeni wajaribu kujipatia vitambulisho vya kupigia
kura wafikia 2040 kwa mikoa ya mikoa ya
Kagera watu 708, Mara 619, Tanga 348,Kigoma 254, Rukwa 13, Kilimanjaro 12,
Ruvuma 9, Geita 6, Shinyanga 7, Mtwara 3, Pwani 2, Mbeya 1, Morogoro 1 na Dar
es Salaam 65.
Hayo yamesemwa na Kaimu kamishna wa uhamiaji Abasi Irovya
wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano ofisini
kwao jijini Dar es Salaam leo.
Aidha Irovya amesema
amewakumbusha wananchi kupiga kura ni haki ya kila mwananchi wa Tanzania ana
sio raia wa kigeni kujiandikisha ili apige kura kwana raia wa kigeni hana uwezo
wa kupiga kura katika nchi asiko zaliwa.
Pia Irovya amesema kuwa wananchi walio chukua paspoti za
kusafiria zinapoisha muda wake ni lazima wabadilishe na kupewa nyingine wakati
wowote wanapohitaji.
Irovya ameongezea
kuwa wananchi wanaotafuta paspoti za kusafiria tofauti na ofisi za uhamiaji
wajue huko wanapotea paspoti zote zinapatikana katika ofisi za uhamiaji tuu na
sio popote pale.
Kutoka kushoto ni Naibu Kamishna wa uhamiaji wilaya ya Iala,
Safina Muhindi,katikati ni Afisa
uhamiaji wilaya ya Temeke, Jaffari Kisesa na Afisa Mdhibiti wa Paspoti,
Cripin Ngonyani wakimsikiliza Kaimu kamishina wa uhamiaji Abasi Irovya wakati
akizungumza na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa mikutano ofisini kwao
jijini Da es Salaam leo.