Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema kuwa Rais wa FIFA Sepp
Blatter anastahili kwa heshima zote kupewa tuzo ya heshima ya Nobel kwa mchango
wake mkubwa katika soka.
Blatter alikutana na Putin siku ya Jumamosi huko St. Petersburg wakati
akitangaza nia thabiti ya FIFA katika kuisapoti Urusi kuandaa kombe la dunia
mwaka 2018.
Na Putin sasa ambaye amekuwa akizungumza kuhusu tuhuma za
rushwa zinazoelekeza kwa Blatter amesema kwamba kwa upande wake haoni kama tuhuma hizo zina ukweli wowote.
“Sote kwa pamoja
tunajua hali inayomkabili Blatter kwa sasa. Sitaki kwenda ndani zaidi ila
sitaki pia kuamini kuhusu tuhuma hizi za rushwa zinazoelekezwa kwake”. alinukuliwa
na RTS.
“Nadhani watu
wanampenda Blatter au mkuu wa taasisi kubwa kabisa ya michezo, au michezo ya
Olimpiki, anahitaji heshima maalum. Kama kuna
mwingine yeyote anayehitaji tuzo hii ya Nobel basi ni watu hao.”