Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa
Arusha, imewaburuza mahakamani vigogo watatu wa Kituo cha Zana za Kilimo na
Teknolojia (Camartec), kwa tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi.
Ilidaiwa mbele ya
Hakimu Patricia Kisinda wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya
Arusha/Arumeru kuwa, watuhumiwa hao walitoa zabuni ya matengenezo ya gari kwa
kampuni ya Mbilinyi Auto Garage ambayo malipo yake yalikuwa Sh. 24,820, 000.
Vigogo walioburuzwa
mahakamani hapo ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Camartec, Elifariji Makongoro,
Ofisa Manunuzi Absalom Nnko na Kaimu Ofisa Usafiri, Pythias Ntella.
Walidaiwa kwa kukiuka
sheria hizo waliisababishia hasara Camartec ya Sh. 24, 820,000.
Hata hivyo,
watuhumiwa hao wote walikana kutenda makosa hayo.
Mahakama ilisema kosa
wanalotuhumiwa watuhumiwa hao lina dhamana na hakimu alitaja masharti kuwa ni
lazima wadhaminiwe na watu wawili wenye vitambulisho kwa kila mmoja na kuweka
bondi ya Sh. milioni 30 au mali
isiyohamishika yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha.
Watuhumiwa wote
walifanikiwa kutimiza masharti na hivyo kupata dhamana hadi Agosti 24, mwaka
huu kesi hiyo itakapoanza kusikilizwa ushahidi wa awali.
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani
Manyara, imemhusisha Mbunge wa Babati Mjini, Kisyeri Chambiri (pichani kulia),
na tuhuma za kutoa hongo katika kura za maoni ndani ya Chama Cha Mapinduzi
(CCM).
Takukuru inadai kuwa
mbunge huyio alinusurika kukamatwa juzi usiku akiwa na wapambe wake waliokuwa
wanagawa rushwa.
Kamanda wa Takukuru
mkoani Manyara, Mogasa Mogasa, alisema Chambiri akiwa na wezake watatu ambao
wanashikiliwa na taasisi hiyo, alinusurika kwa kutimua mbio usiku majira ya saa
nne na kuacha kitita chaSh. 500, 000 alizokuwa nazo katika kijiji cha Kiongozi
akitaka kuzigawa kwa baadhi ya watu wake.
Pia taarifa ya
kamanda huyo ilieleza kuwa Chambiri alifanikiwa kukimbia akiwa na viongozi
kadhaa wa kijiji hicho ambao kamanda huyo hakuta kuwataja majina, akisema kuwa
wanaendelea kutafutwa na kumtaka Chambiri ajisalimishe.
Kamanda huyo
aliwataja waliyokamatwa kuwa ni Samuel John Barani ambaye ni Katibu wa Uchumi
na Fedha CCM wilaya; Thomas Cosmas Darabe na Ally Ayubu Ramadhani, ambao
walikuwa na mgombea huyo katika harakati hizo.
Kamanda Mogasa
paliongeza kuwa baada ya watuhumiwa hao kukutwa katika eneo hilo na Chambiri kutokomea, walifanikiwa pia
kukamata makaratasi yenye majina ya watu waliokuwa wameandaliwa kwa ajili ya
mgawo huo.
Hata hivyo, alisema
wanaendelea na mahojiano watuhumiwa hao na kwamba baada ya taratibu kukamilika
watafikishwa mahakamani na kuongeza kuwa wanalishikilia gari la mbunge huyo.
Chambiri alipoulizwa,
alikana kuhusika na kudai kuwa ni mbinu zinazotumiwa na baadhi ya watu
wasiyomtakia mema.
Aidha, alidai kuwa
yeye kama mgombea na mtetezi wa jimbo hilo ,
amekuwa akipata taarifa mara kwa mara za kupangiwa njama kama
hizo ili kudhoofisha juhuddi zake za kurejea madarakani.
“Hivi walishindwaje kunikamata wakati wanadai walitukuta
tukiwa ndani kama siyo uzushi, mimi nafahamu kuna watu wamewekwa kunichunga
hata kama naenda nyumbani kisa tu mimi
nisichanguliwe, na hiyo ni baada ya kuona watu wameonyesha upendo kwangu,”
alisema Chambiri