Mabaki hayo yaliyopatikana yanapelekwa Ufaransa kwa uchunguzi
zaidi ili kubaini kama ndege ya Malaysia
iliyopotea Boing 777,MH 370 iliyokuwa ikitoka Quala lumpa Malaysia ikielekea Beiging China
Machi mwaka jana.
John Begue ni mfanyakazi wa fukwe za Saint Andre na ndiye
aliyeona mabaki hayo kwa mara ya kwanza,akihojiwa na vyombo vya habari anasema
aliona kitu kama mzigo "siku ya
Jumanne asubuhi wakati nafanya kazi katika eneo langu nikiwa natafuta mawe kwa
ajili ya shughuli zangu ndipo nilipoona kipande cheupe kinachofanana na mabaki
ya ndege ambacho nusu yake ilikua ndani ya maji na nusu yake kwenye
mchanga.Kukiwa na hali ya upepo baharini ,niliwaita wafanyakazi wenzangu
kunisaidia kukibeba kipande hicho na ndipo nilipoona pia sanduku lakini
sikulitilia maaanani bali akili yangu ikawa zaidi kuchunguza kipande cha ndege
nilichokiona ni muhimu kwangu''
Ndege hiyo ya Malaysia ambayo ilipotea miezi sita
iliyopita ilikuwa imebeba abiria 239,ushahidi huu wa mabaki huenda ukawa wa
kwanza kufuatilia jitihada za muda mrefu kujua undani wa ajali hiyo.