Liwalo na liwe! Kinara wa sinema za Kibongo, Jacqueline
Wolper Massawe ameahidi kuambatana na waziri mkuu wa zamani ambaye ni Mbunge wa
Monduli kwa leseni ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Edward Ngoyai Lowassa kwenye
safari yake ya kuhamia kwenye muungano wa vyama vya upinzani vinavyounda Umoja
wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, wikiendi iliyopita, Wolper
alisema kwa mapenzi aliyonayo kwa Lowassa yupo tayari kwenda kokote hata kama siyo Ukawa.
“Mimi ni ‘Team Lowassa’, atakapohamia nami niko nyuma yake
hata kama siyo Ukawa, nitamfuata, mimi na Lowassa ni damdam, hilo halina ubishi,” alisema Wolper.