Polisi nchini Afrika kusini wanamtafuta mwanamme mmoja
ambaye analaumiwa kwa kumuua mkewe kwa kutumia gurunedi.
Inadaiwa kuwa wawili hao walikuwa wakijibizana wakati
mwananme huyo alimtupia mkewe gurudeni mbili ambapo mojawapo ililipuka.
Mwanamke huyo aliaga dunia saa chache baadaye katika
hospitali ya kingsway mjini Durban kutokana na
majeraha aliyoyapata kutokana na mlipuko huo ambao pia uliharibu sehemu ya
nyumba yao .
Mwanamme huyo anashukiwa kuwa mwanajeshi katika jeshi la
Afrika Kusini.
Polisi wa kutegua mabomu walipata moja ya magurunedi hayo
ambalo halikuwa limelipuka na kuliondoa eneo hilo .