Maafisa wa serikali nchini Nigeria
wamesema kuwa kundi la wapiganaji wa Kiislamu wa Boko Haram, wanajaribu kupanua
shughuli zao kutoka maeneo ya Kaskazini, yenye idadi kubwa ya Waislamu, hadi
mji mkuu wa Lagos
na maeneo mengine.
Wakakti huo huo idara ya ujasusi nchini humo imesema kuwa
imewakamata takriban makamanda 20 wa kundi hilo la Boko Haram, Aidha idara hiyo
imesema kuwa wapiganaji wengine wamekamatwa katika majimbo yaliyo Kaskazini mwa
nchi ya Kano, Gombe , Central Plateau, pamoja na maeneo ya Lagos Kusini na
Enugu kati ya Julai na Agosti mwaka huu.
Taarifa hiyo kutoka kwa idara ya huduma za kitaifa inasema
kuwa wapiganaji hao wa Boko Haram wameanza kuhamahama kutoka ngome zao kwa
sababu ya shinikizo kutoka kwa vikosi vya usalama katika maeneo ya Kaskazini
Mashariki mwa nchi.