Wacha tusemezane kidogo...na leo tusemezane juu ya hii
silaha ya maangamizi ya ndugu Lowassa.
Ikiwa Lowassa na Mbowe wataweza kuhakikisha Slaa anaendelea
kunyamaza, nini itakuwa athari kwa mbio zao kuelekea Magogoni? Hii itaendelea
kuwaaminisha wale walioamua kufa kishujaa na Slaa na wale ambao bado hawajaamua
nani wampigie kura waendelee kuamini kuwa Lowassa ni Fisadi na hafai kuwa Amiri
Jeshi wa Majeshi yetu.
Ila Mbowe na Lowassa endapo watazichanga karata zao vizuri
na kumuangukia Slaa na Slaa hata akaamua kushiriki katika Campaign japo
kishingo upande, basi CCM wategemee upinzani mkali ambao hawajawahi kuupata
tangu kuzaliwa kwa chama hicho.
Ila endapo Mbowe na Lowassa wakampuuza Slaa kwa kuamini kwamba
hana impact yeyote eti kisa tu watu wanataka Mabadiliko, basi endapo Slaa
ataamua kuufungua mdomo wake kuongea na Watanzania, Mbowe na Lowassa wategemee
anguko kuu ambalo halijawahi kuonekana katika nchi hii.
Tujaribuni kusemezana kistaarabu tu, kama
Mbowe na Lowassa wanavyohubiri namna Campaign zitakavyoendeshwa bila ya matusi,
basi na hapa tusemezane tu bila Matusi.