Mtu mmoja amefariki dunia na mwingine kujeruhiwa wakati watu
wanaosadikiwa kuwa ni majambazi waliposimamisha daladala eneo la Jangwani na
kuingia ndani kupora mkoba unaosadikiwa kuwa na fedha.Askari na wasamaria wema
wakiwa wamebeba mwili wa abiria aliyepigwa risasi na majambazi akiwa ndani ya
daladala eneo la Jangwani, Dar es
Salaam jana.
Daladala hilo
lilikuwa likitoka Kariakoo likielekea Ubungo Mawasiliano. Picha na Edwin
Mjwahuzi Watu hao, waliokuwa na pikipiki aina ya boxer, walikuwa wakifuatilia
basi hilo
linalofanya safari zake kati ya Kariakoo na Mwenge na kulisimamisha eneo la
Jangwani saa 7.30 mchana na baadaye kuwaamuru abiria wote wainame kabla ya
kuelekea kiti cha nyuma alikokuwa amekaa mtu huyo aliyekuwa amebeba mkoba.
Mmoja wa abiria wa daladala hilo , Rehema Michael alisema wakati basi lao
likiwa linaenda taratibu, alimuona mtu aliyekuwa amepakizwa kwenye pikipiki
akishuka na kumfuata dereva na kisha kumuelekezea bastola usoni, akimtaka
asimamishe gari.
Alisema dereva wao alitaka kukunja kona kuelekea Jangwani,
lakini akatii amri na ndipo dereva wa bodaboda alipokwenda nyuma ya daladala na
kumtaka mmoja wa abiria aliyekuwa amekaa nyuma ya daladala kutoa begi, huku
mwingine akipiga risasi hewani, lakini hakupewa mkoba huo.
“Baada ya kuona yule abiria anakaidi agizo lao, mmoja wa
majambazi hao alimpiga risasi ya kichwani na kifuani na kuanguka chini huku
yule abiria mwenzake ambaye alipewa begi hilo
alishike alilitupa chini na mmoja wa majambazi aliingia ndani ya daladala na
kulichukua,” Hashim Ally.
Shuhuda mwingine, Richard Urio alisema wakati uvamizi huo
ukitokea abiria walikuwepo ndani ya daladala hiyo akiwemo konda walilazimika
kulala chini baada ya kusikia milio ya risasi zilizokuwa zikipigwa hewani, na
kwamba baada ya kuchukua lile begi walimpiga risasi abiria mwingine ambaye
alikuwa karibu na marehemu baada kuhisi alikuwa akizuia begi lisitolewe.
“Siti ya nyuma walikuwa wamekaa abiria wanne, na wawili kati
yao walikuwa
wamasai ambao mmoja wapo alikuwa amevaa begi mgongoni ambalo lilichukuliwa na
majambazi baada ya kumuua mmoja wa wamasai huku mwingine akijeruhiwa na bastola
shavuni,”Urio.
Shuhuda mwingine, Regina Mateso alisema yeye alipanda
daladala hiyo eneo la Shakilango na kuwakuta wamasai hao ambao inasemakana
walikuwa na fedha nyingi kutokana na maongezi yao .
“Wale wamasai walikuwa wanapigiana mahesabu na wapi kwa
kwenda kubadilisha fedha. Yule aliyefariki alikuwa anamwambia mwenzake
ukibadilisha hizi dola unapata Sh16 milioni, hivyo inawezekana wale abiria
walikuwa na kiasi hicho cha fedha ambacho walikuwa wameweka katika begi la
mgongoni,” Mateso.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Polisi Ilala, Lucas Mkondya
alisema tukio hilo
limetokea na wanalifanyia kazi .
“Na sisi polisi tumelipata sasa hivi ndio kwanza
tunalifanyia kazi likikamilika tutatia taarifa,” Mkonya