UTANGULIZI
Sheria hii ya makosa ya mtandao, 2015 imebainika kuwa na
mapungufu
makubwa sana .
Mapungufu hayo yamebainika kuwa, kama sheria
ikipita
yanaweza kuifanya nchi ikawa ni kati nchi adui za matumizi
ya mtandao
wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano duniani.
Watanzania wote wanatakiwa kufahamu kuwa muswada ukipita
utatumika nchini kote yani Tanzania Bara na Visiwani.
Watanzania walio wengi hawafahamu Sheria hii inawahusu kwa
namna
gani; lakini kwa lugha rahisi ni kuwa itamuathiri mtu yeyote
anayeweza
tumia mtandao wa intaneti kwa kutimia kifaa chochote iwe
kompyuta
kubwa au vifaa vyenye uwezo wa kufanya kazi kama kompyuta kama
Simu za mikononi, saa, televisheni na vifaa vingine
vinavyoendana na
hivyo.
Malengo ya Sheria hii ni kuainisha makosa yanayohusiana na
matumizi
ya mfumo wa kompyuta na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano,
kuweka utaratibu wa upelelezi, ukusanyaji na matumizi ya
ushahidi wa
kielektroniki na masuala mengine yanayohusiana na hayo.
Matumizi ya mitandao yote mikubwa kama
Twitter, Instagram,
JamiiForums, Facebook, Barua pepe, WhatsApp, blogu na data
zote
zilizo katika kifaa chochote cha kielektroniki yanaathiriwa
kwa kiwango
kikubwa na Muswada huu.
UCHAMBUZI
Ibara ya 4
Ni computer gani inazungumziwa hapa? Ya nani?
Ibara ya 5
Computer gani inayokusudiwa, ya nani?
Ibara ya 7
(1-3): Haibainisha ni aina gani za data ambazo haziruhusiwi
kuguswa/kufutwa au zikiguswa/futwa ni kosa la jinai.
7(1g): Kipengele hiki katika ibara hii kinarudiwa mara
kadhaa katika
(Ibara za 32-35). Badala ya ibara za mbele kurejea ibara
hii, watunga
sheria wameiacha ibara hii ikiwa haieleweki hadi mtu asome
ibara za
mbele.
Je mtu
aliyeidhinishwa katika ibara na kipengele hiki ni nani?
Ibara ya 8:
Muswada huu haujaweka bayana iwapo nyaraka za siri zinaweza
kuwekwa wazi katika mtandao kama
zina maslahi ya nchi au wananchi
mf. Matumizi mabovu ya pesa za umma
Ibara ya 14:
Neno pornografia halijapewa maana na hivyo jambo lolote
lenye
mwonekano wa kiasherati (sexually vulgar) linaweza
kutafsiriwa kama
pornografia na kumuingiza muhusika matatizoni.
Ponografia ya mtandao isikatazwe kabisa ila inatakiwa kuweka
ulinzi
thabiti wa kuhakikisha watoto hawawezi kufungua mitandao ya
aina
hiyo.
Ponografia zote ni chafu lakini sio chafu zote ni ponorafia.
Hivyo
kutokana na kuwa sheria hii inasema ponografia zote ni chafu
hii
itasababisha kila mtu ahukumiwe chini ya kifungu B.
Uchafu na Ponografia
viwe vipengele viwili tofauti.
Artcile 15:
Suala la kujifanya mtu mwingine kwenye mtandao, linaweza
kuleta utata
kwani kuna baadhi ya mitandao ambapo watumiaji hutumia
majina
ambayo sio ya kwao. Itakuwaje watu kwa madhumuni mabaya
wakitafuta
mtu mwenye jina kama hilo
na kumshtaki mtumiaji wa mtandao?
Je, mtu kujifanya mtu mwingine inahusisha mtu kutumia jina
lisilo lake
hata kama hajajifanya mtu
mwingine? Ni vema suala hili likafafanuliwa
kisheria kwakuwa ni suala muhimu lakini wachache wataelewa
manaa
yake.
Ibara ya 16:
Ni nani ana mamlaka ya kubainisha kuwa jambo lililowekwa
kwenye
mtandao ni la UKWELI, UONGO au UPOTOSHAJI? Ni wazi kuwa
mamlaka husika inaweza tumia hili kama mtego kwa manufaa yao .
Kipengele hiki kama vingine
kimeambatanisha muda usiopungua bila
kusema muda usiozidi. Hivyo mtuhumiwa anaweza kufungwa hata
kifungo cha maisha kutokana na mamlaka ya mahakama.
Watu binafsi wanaweza kutumia vibaya kifungu hiki kuzuia
uhuru wa
maoni kwa kuwaburuza watumiaji wa mtandao mahakamani kila
kukicha
na kuwapotezea muda wahusika ambao wanaweza kubainika
mwishoni
kuwa walionewa.
Ibara ya 20:
Katika mawasililano ya mtandao kama
ilivyo mawasiliano mengine kuna
ujumbe ambao mtu hawezi kuacha kuupata
Mfano kutembea barabarani na kuona bango la matangazo, au
kuwa
ndani ya daladala iliyowasha redio.
Vivyo hivyo katika mtandao sio kila ujumbe anaopokea
mpokeaji
ameuomba na hivyo kifungu hiki kinafanya kila mtu
atakayepokea
ujumbe bila ridhaa yake kuwa amefanya kosa la jinai.
Ibara ya 21(1):
Tafsiri za Kiswahili na kiingereza zipo tofauti kabisa.
Ya Kiswahili inamlenga mtoa huduma na huku ya kingereza
inamlenga
mtu yeyote anayetumia mtandao.
Ya Kiswahili inamlazimu mtoa huduma kumtaja mhusika
aliyeweka
ujumbe na pia kumuadhibu mtoa huduma huku ya kiingereza
inazungumzia kuhusu tafiti kwa ujumla.
Ya kiingereza ni nzuri lakini ya Kiswahili imepotoshwa
kabisa na
inavunja uhuru wa mawasiliano.
MUHIMU:
Hakuna kinga yoyote kwa mtoa taarifa (source) kwa mujibu wa
ibara hii.
Ibara ya 22:
Je, nani ana mamlaka ya kuamua kuwa ujumbe kwenye mtandao
unatolewa au kuboreshwa kwa kusudi au bila kusudi.
Itambulike kuwa ujumbe wa kwenye mtandao huboreshwa (edit)
au
kufutwa wakati wowote muhusika anapoona inafaa mf. Whatsap
status,
fb status etc.
Ibara ya 23:
Unyayasaji wa kupitia mtandao (cyber bullying) haujapewa maana.
Sheria inatakiwa kuweka bayana maudhi ya kihisia ni nini.
Kwani mtu yeyote atakayeudhiwa ‘kihisia’ au kudai kuwa hisia
zake
zimeudhiwa anaweza kushtaki. Sio kila linalosababisha maudhi
ya kihisia
ni unyanyasaji
Ibara ya 27:
Ni nani anaamua kitendo fulani ni kula njama? Mazungumzo ya
kawaida
na maamuzi ya kukubalika na upande mmoja yanaweza
kutafsiriwa kama
kula njama na watu wa upande mwingine.
Ibara ya 31 (3a):
Sheria ya kiingereza inasema ‘as soon as practicable’ lakini
ya
Kiswahili inasema wakati wa upekuzi na ukamataji wa mali . Hizi zina
maana tofauti.
Ibara hii inawapa mamlaka Wakuu wa Vituo vya Polisi kufanya
upekuzi
na kuchukua mali (za
kielektroniki) na taarifa binafsi za raia bila amri ya
Mahakama.
Ibara ya 32-35
Ibara hizi zinamlazimisha mtoa huduma kutoa data za wateja
wake kwa
Mkuu wa kituo cha Polisi bila kibali cha Mahakama. Wakuu wa
Vituo
vya Polisi wamepewa nguvu sana katika sheria hii! Mahakama ipewe
mamlaka haya na si Polisi, na ifanyike hivi baada ya
kujiridhisha kuwa
mwananchi anatakiwa kufanyiwa upekuzi, kuchukuliwa data zake
au za
wateja wake n.k
Ibara ya 39-45
Watoa huduma na wahifaji tovuti wanalindwa na ibara hizi
lakini kwa masharti.
Katika ibara ya 39, Waziri anapewa mamlaka ya kuamua kipi ni
kosa na kipi si kosa.
Anapewa mamlaka ya kusimamisha na kusitisha huduma, kuondoa
taarifa juu ya kitendo
husika (mfano kulazimisha kuondoa mijadala yote ya ufisadi
flani kama yeye ataona kwa
mamlaka yake kuwa haufai kujadiliwa).
Muswada huu ibara za 31-38 na ibara za 39-46 zinakinzana
kwani kwa wakati mmoja mtoa
huduma anaweza akawa ameona jambo ameshalitoa na anajiandaa
kuitaarifu mamlaka husika
huku mamlaka husika (Askari Polisi) ikiwa na uwezo wa kwenda
kuchukua vifaa na data za mtoa huduma.
Mamlaka ya Polisi imepewa kinga kubwa ambayo haiingiliani na
sheria yoyote ile.