Maelfu ya watu wanashiriki katika siku ya pili ya maandamano
ya kupinga serikali kwenye mji mkuu wa Malaysia
Kuala Lumpur .
Mamia walikesha kwenye mitaa usiku kucha. Polisi wametangaza
maandamano hayo kuwa haramu lakini hawajachukua hatua za kuyavunja, Pia
kumekuwa na maandamano katika miji mingine ya nchi hiyo lakini yamekwisha..
Wanaharakati nchini humo wanataka waziri mkuu nchini
Malaysia Najib Razak ajiuzulu.
Wanaamini kuwa hajaelezwa vilivyo ni kwani nini akaunti zake
ya benki zilipataika zikiwa na mamilioni ya dola.