Maelfu ya waandamaji wanaopinga serikali wamekusanyika
katika nji mkuu wa Malaysia ,
Kuala Lumpur
wakitaka waziri mkuu Najib Razak ajiuzulu kwa madai ya ufisadi yanayomkabili.
Mkutano huu wa hadhara umekuwa ukiendelea kwa siku mbili
sasa hata baada ya polisi kuupiga marufuku.
Waandamanaji hao pia walikiuka amri rasmi ya kutovaa nguo za
manjano zinazotumika na kundi ambalo limeandaa maandamano hayo.
maandamano hayo yalianzishwa baada ya zaidi ya dola milioni
mia moja kupatikana katika akaunti ya kibinafsi ya waziri mkuu. Amesisitiza
kuwa pesa hizo zilikuwa za msaada na akakanusha kufanya kosa lolote.