Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia
chama cha Mapinduzi (CCM),Dkt John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi wa
Njombe mjini katika mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika jioni ya leo
katika uwanja wa saba saba.Magufuli amesema akichaguliwa kuwa rais wa awamu ya
tano ataendeleza juhudi zake za kujenga barabara kwa kiwango cha lami,amesema
dhamira yake aliokuwa nayo ya Uwaziri wa Ujenzi katika kujenga barabara za lami
katika maeneo yote hapa nchini.
Dkt MAGUFULI ambae anaendelea na mikutano ya kampeni za
Urais mikoa ya nyanda za juu kusini , amelalamikia udanganyifu wa baadhi ya
mitandao ya kijamii na baadhi ya vyombo vya habari kuripoti kuwa amelazwa wodi
ya wagonjwa mahututi katika hospitali ya mkoa wa mbeya wakati sio kweli.
Amesema tangu kupewa kuwa waziri wa ujenzi ameweza kujenga
barabara zaidi kilomita 7000 nchi nzima,ambapo ilipelekea kuongeza kuongeza
pato la mfuko wa barabara kutoka bilioni 73,3 hadi kufikia bilini 866 kwa mwaka
huu hivyo ameahidi akiwa rais atajenga zaidi barabara za lami.
Aidha pia Magufuli amewaomba wananchi waweke imani kubwa
kwake kwa kumpa kura nyingi zitakazomwezesha kuwa raisi wa awamu ya tano,na
kIsha alipe fadhira hizo kwa kutatua kero zinazowakabili hasa wananchi wenye
kipato cha chini