Wasichana wasiopungua 38 wamefariki dunia katika ajali ya
barabarani wakiwa njiani kwenda kumchezea Mfalme Muswati III wa Swaziland katika sherehe za kila mwaka
zinazowashirikisha maelfu ya wasichana ambao mfalme huyo huchagua mke wake mpya
baina yao .
Vyombo vya habari nchini Swaziland vimeripoti kuwa wasichana
hao wamepata ajali barabarani baada ya basi lao kugongana na gari jingine.
Wasichana hao walitazamiwa kushiriki katika sherehe ya kesho Jumatatu ambapo
makumi ya maelfu ya wasichana bikira watashiriki na kucheza mbele ya Mfalme
Muswati III kabla ya kuchagua mmoja wao kuwa mke mpya. Mflme Muswati III
ameitaja ajali hiyo kuwa ni maafa ya kitaifa.
Vyombo vya habari vya Swaziland vimezuiliwa kupiga na
kuonesha picha za ajali hiyo.
Mfalme Muswati III mwenye umri wa miaka 47 ana baina ya
wanawake 13 na 15.