F Ugonjwa wa Kipindupindu | Muungwana BLOG
https://c2p.cleverwebserver.com/dashboard/6a0bec4b-79ba-11ef-ad2b-06f0639468d1

Ugonjwa wa Kipindupindu

Kipindupindu ni ugonjwa wa ghafla  wa  kuhara unaosababishwa na kula chakula au kunywa  maji/vinywaji vyenye vimelea/ bakteria waitwao Vibrio cholera . Watafiti wanakadiria  kuwa kila mwaka, kuna kesi  takribani  milioni 1.4-4.3  na vifo  28 000-142 000 vinavyotokana na ugonjwa wa Kipindupindu. Muda mfupi  wa maambukizi ni sababu moja wapo  ambayo husababisha kuenea kwa mlipuko wa kipindupindu.

Mtu hupata maambukizi ya kipindupindu baada ya kutumia chakula au maji yaliyo chafuliwa na kinyesi cha mtu mwenye vimelea wa kipindupindu. Vifuatavyo ni vyanzo vya maambukizi

•Vyanzo vya maji yaliyochafuliwa na kinyesi cha binadamu
•Barafu zilizotengenezwa kutokana na maji machu
•Vyakula au vinywaji vinavyouzwa mtaani
•Mbogamboga ambazo zinamwagiliwa maji yaliyochafuliwa na kinyesi cha binadamu
•Kula samaki wabichi au ambao hawakuiva vizuri na wametoka katika maeneo ambayo yanachafuliwa na kinyesi cha binadamu.

Dalili za  Kipindupindu
Kipindupindu ni ugonjwa wa hatari  sana. Dalili  hujitokeza kati ya masaa mawili mpaka siku tano baada ya kupata maambukizi.  Ugonjwa huu huathiri watu wa rika zote watoto na watu wazima. Kipindupindu   kinaweza kuua ndani ya masaa machache baada ya  dalili kujitokeza.

Asilimia 80  ya watu walioambukizwa vimelea wa kipindupindu hawaonyeshi dalili yoyote.Hata hivyo  mtu  ataendelea kutoa bakteria katika kinyesi chake kwa muda wa siku 1-10 baada ya kuambukizwa na hivyo kusababisha bakteria  hao kusambaa katika mazingira hivyo kuongezeka  uwezekano wa kuwaambukiza watu wengine.

Miongoni mwa watu ambao huonyesha dalili, 80% huwa na dalili kiasi  au wastani, wakati 20% wana harisha majimaji kwa wingi na kupata upungufu mkubwa wa maji mwilini. Hali isipotiwa huweza kusababisha kifo.

Maambukizi ya Kipindupindu  yana mauhusiano ya  karibu na usimamizi duni wa mazingira. Mfano   maeneo ambayo yako katika hatari ni makazi duni pamoja na maeneo yaliyoko kandokando mwa miji, ambapo miundombinu ya msingi haipatikani, na pia maeneo ya makambi ya wakimbizi, ambapo mahitaji ya kimsingi ya maji safi na usafi wa mazingira ni hayapatikani kwa urahisi.


Migogoro katika  jamii  uhaba wa mifumo ya maji na usafi wa mazingira, Makambi ya wakimbizi au makazi yenye msongamano mkubwa wa watu inaweza kuongeza hatari kuenea  kwa  maambukizi ya kipindupindu

Kipindupindu bado ni  tishio duniani kwa afya ya umma na ni  kiashiria muhimu cha ukosefu wa maendeleo ya kijamii.

Matibabu
Kipindupindu ni ugonjwa ambao unatibika urahisi . Asilimia 80 ya wagonjwa wanaweza kutibiwa kwa ufanisi kwa kutumia  dawa za majimaji (WHO / UNICEF ORS) . Wagonjwa wenye upungufu mkubwa wa maji mwilini huitaji kuongezewa maji ya drip kwa njia ya  mshipa. Wagonjwa hawa pia huitaji antibiotics sahihi ili kupunguza muda wa kuhara, kupunguza kufupisha muda wa bacteria wa kipindupindu kutolewa kwenye kinyesi.

Hata hivyo, unaweza kujikinga wewe pamoja na familia yako kwa kutumia maji ya chupa ,maji ambayo yamechemsha, maji ambayo yametiwa kemikali ya kuwa vijidudu.Hakikisha kuwa  unatumia maji ya chupa, kuchemsha, au yaliyotiwa kemikali kwa madhumuni yafuatayo:
•Maji ya kunywa
•Kuandaa chakula  au vinywaji
•Kutengeneza Barafu
•Kuosha vyombo vya chakula
•Kuosha matunda
•Kupiga mswaki