RAIA wa China ,
Jianfeng Wu amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na
mashitaka ya kukutwa na meno ya simba yenye thamani ya Sh milioni 10.1.
Baada ya kusomewa mashitaka, mshitakiwa hakuruhusiwa kujibu
mashitaka kwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo ya
uhujumu uchumi isipokuwa Mahakama Kuu.
Awali, wakili wa Serikali, Paul Kadushi alidai mbele ya
Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha kuwa ilikuwa Agosti 18, mwaka huu katika
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Wu alipokamatwa akiwa na meno
matatu ya simba.
Hakimu Mkeha aliahirisha kesi hiyo hadi Septemba 10, mwaka
huu itakapokuja tena mahakamani hapo kwa hatua nyingine.