Kuna watu wanajaribu kupotosha nini hasa mantiki ya Mgombea
Edward Lowassa kuahidi kushughulikia suala la Sheikhs wa Zanzibar na suala la Babu Seya.
Suala la Sheikhs wa Zanzibar
liliihusisha Chadema kabla hata Lowassa hajahamia huku. Binafsi niliombwa na Dr Slaa
kulishughulikia, lakini bahati mbaya nilikuwa nina cases kadhaa zilizonifanya
nikwame. Lakini cha muhimu zaidi ni kwamba wana Wakili, tena Wakili mahiri tu
na ambaye ni Mwanachama wa Chadema. Amepambana sana , na anaendelea mpaka leo.
Issue yao
ni complicated, na ni mfano tu wa issues zinazo athiri haki za wananchi kwa
kukosekana tu utashi sahihi wa kisheria na kiutawala.
Mojawapo wa pertinent issues ni mgogoro wa iwapo wanatakiwa
kishtakiwa Bara, au Zanzibar
inakosemekana walitenda huo ugaidi.
Na kuna masuala ya Sheiks wale kulalamika kutendewa kinyume
wakiwa chini ya ulinzi.
Kuna suala pia la ucheleweshaji wa upelelezi, hata kama
tuna-assume case dhidi yao
ina mashiko.
Asiyefahamu anaweza kudharau uzito wake, lakini ni suala
linaloleta hisia kali kwa sehemu ya waumini wa kiislamu.
Lowassa atakuwa Rais wa ajabu kama vision yake ya kisheria
haitajumuisha suala pertinent kama hilo .
Huwezi jadili general concepts bila kuchagua specifics kadhaa kama
mfano.
Pia, Lowassa hajasema atamtoa Babu Seya kwa stroke ya pen on
a whim. Wala hajasema hiyo ni priority yake above all else kwa upande wa
sheria. Alichosema within the limited confines za muda ni kwamba serikali yake
itakuwa makini sana
na masuala ya utawala wa sheria. Issue ya Babu Seya na hao Sheiks ni
representation tu ya matatizo yaliyopo. Na malalamiko yaliyopo. Issue ya
Lawrence Masha na wale vijana 19 wa 4U Movement tuliowapigania juzi, imepigia
mstari.
Pamoja na kwamba ni suala linalogawa opinion, ni naivety
kujidai eti issue ya Babu Seya si moja ya issues zinazoleta mjadala wa kisheria
na kihisia mpaka leo hii. Suala la ni namna gani linashughulikiwa, ni suala la
ushauri wa kisheria kutoka kwa wataalamu wa Rais Lowassa (kipindi hicho).