Wananchi wa Libya
wamefanya maandamano wakilalamikia hali ngumu ya maisha na kuongezeka umaskini
nchini humo. Wananchi hao waliandamana leo mbele ya Kongresi ya Taifa ya nchi
hiyo huko Tripoli
na kutaka kulipwa fidia familia zote zilizoathirika katika mapinduzi ya mwaka
2011 dhidi ya utawala wa Kanali Muammar Gadafi.
Washiriki katika maandamano hayo wametaka Benki Kuu ya nchi
hiyo ishinikizwe ilipe haraka fidia hizo kwa familia ambazo sasa zinateseka na
hali ngumu ya maisha.
Maandamano hayo yaliwajumuisha wakazi wa miji ya Misrata, al
Zawiya, al Khamis, Zeltan na Sabrata. Washiriki katika maandamano ya leo ya
mjini Tripoli Libya wamesema kuwa familia karibu
elfu 11 za nchi hiyo ziliathirika vibaya katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo
wakati wa mapinduzi ya tarehe 17 Februari mwaka 2011.