JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam likishirikiana na Mkoa wa Pwani
na mikoa mingine ya jiarani limefanikiwa kuwakamata watu 38 wanaojihusisha na
vitendo vya kigaidi.
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam,Kamanda wa
Kanda Maalum ya Kipolisi Dar es Salaam, Suleiman Kova, amesema kuwa
katika oparesheni ya pamoja na Mkoa wa Pwani kwa kutumia vikosi maalum
wamefanikisha kuwakamata hao nyakati
tofauti na kukutwa na bunduki aina ya
SMG 02, SAR 02,Shot gun sita, risasi 310 za SMG/SAR, risasi 37 za G3, risasi 40
za Shot gun, bomu moja la kurushwa kwa
mkono.
Aidha alisema walikamata vifaa vya kutengenezea milipuko
sita, Charger sitaza kuhifadhia risasi
na waya wa kuunganisha mabomu na vifaa mbalimbali.Kova alisema ili kuthibitisha kuwa wahalifu hao si wa
kawaida wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali za kuficha silaha hizo au wao
wenyewe kujificha ili wasigundulike .
Kamanda Kova alidai kuwa kutokana na uwezo, weredi na
ushirikiano uliojengeka kati ya jeshi la polisi na raia wema, wahalifu na
sialaha hizo waligundulika wanapojificha
na sehemu zilipokuwa zimechimbiwa ardhini kwa kuwekwa makasha mbalimbali.
“Miongoni mwa silaha tulizokamata ni za kituo cha polisi cha Kimanzichana Wilaya ya Mkuranga,
Pwani, na kituo cha polisi cha Ikwiriri, Pwani, na watuhumiwa wote tunayahifadhi majina yao kwa ajili ya usalama
ili kuendelea kutusaidia kuwataja wengine,” alisema Kamanda Kova.