Benki ya CRDB imetoa msaada wa vifaa tiba na dawa za ugonjwa
wa kipindupindu kwa Manispaa ya Kinondoni.
Akikabidhi msaada huo jana, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Dk.
Charles Kimei, alisema benki yake hutenga asilimia moja ya faida yake kila
mwaka ili kusadia jamii ikiwamo kutembelea maeneo yenye mahitaji kama vile hospitali, shule na vituo vya watoto yatima.
Alisema benki yake imeamua kutumia Wiki ya Huduma kwa Wateja
kutoa msaada huo wenye thamani ya Sh. milioni 15.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Mussa Natty, alisema
msaada huo utanusuru maisha ya Watanzania waliokumbwa na maradhi hayo.
Alisema hadi sasa watu 17 wamepoteza maisha yao
kutokana na maradhi hayo.