Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (katikati),
akizungumza na wafanyakazi wa Gereji ya Spring City Enterprises inayomilikiwa
na raia wa China iliyopo Mikocheni B Mlalakuwa
Barabara ya Mwai Kibaki Dar es Salaam leo, alipofika kusikiliza
malalamiko yao mbalimbali yakiwemo ya kutokuwa na mikataba ya kazi licha ya
kuwa kazini kwa zaidi ya miaka saba.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (katikati),
akizungumza na wafanyakazi wa Gereji ya Spring City Enterprises inayomilikiwa
na raia wa China iliyopo Mikocheni B Mlalakuwa
Barabara ya Mwai Kibaki Dar es Salaam leo, alipofika kusikiliza
malalamiko yao mbalimbali yakiwemo ya kutokuwa na mikataba ya kazi licha ya
kuwa kazini kwa zaidi ya miaka saba.
Makonda akiangalia kitambulisho dhaifu wanavyotumia wafanyakazi hao ambacho hakiwezi kutumimika kumuwekea mtu dhamana na shughuli mbalimbali.
Ofisa Uhamiaji wa Wilaya ya Kinondoni, Evarist Mlay
akizungumza na waandishi wa habari eneo la tukio baada ya kuwepo madai ya
baadhi ya wachina kuishi nchini kinyemela.
DC Makonda (kulia), akiangalia bomba la maji wanayotumia
wafanyakazi hao kwa kunywa. Hata hivyo wafanyakazi hao walilalamikia maji hayo
kuwa si salama kwa kuwa yanatoka eneo la chooni.
Kiongozi wa gereji hiyo, Mr Yu Viangqian (kushoto),
akizungumza na wanahabari kuhusu madai ya kuwanyanyasa wafanyakazi wa
kitanzania na kutokuwa na mikataba.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda leo amefanya ziara
ya kusitukiza katika Karakana ya kutengeneza magari ya Spring City Enterprises
inayomilikiwa na raia wa China iliyopo Mikocheni B Mlalakuwa Barabara ya Mwai Kibaki na kukumbana na
changamoto kadhaa kutoka kwa wafanyakazi wa karakana hiyo.
Makonda akiangalia kitambulisho dhaifu wanavyotumia wafanyakazi hao ambacho hakiwezi kutumimika kumuwekea mtu dhamana na shughuli mbalimbali.
Moja ya changamoto kubwa aliyoelezwa na wafanyakazi hao ni
kutokuwa na mikataba ya kazi na kukosekana kwa huduma zingine anazopaswa
kuzipata mfanyakazi.
Wafanyakazi hao walimwambia Makonda kuwa hawana muda wa
kupumzika wala malipo ya ziada ikiwa na mazingira ya kazi yasiyo rafiki.
Makonda baada ya kupokea malalamiko hayo aliutaka uongozi wa
viwanda hivyo kurekebisha mfumo wao wa kazi ambapo aliwataka watoe mikiataba ya
ajira kwa wafanyakazi hao pamoja na kuboresha mazingira ya kazi na maslahi yao .
Akizungumza na wanahabari Kiongozi anaye simamia karakana
hiyo ya kutengeneza magari ya wachina, Mr Yu Viangqian alisema hakuna haki
yoyote inayokiukwa katika karakana hiyo kwani wao wamejikita zaidi kutoa
mafunzo ya ufundi kwa vijana wa kitanzania na ajira.
"Hakuna jambo baya hapa kwetu sisi tunasaidia vijana
wengi kupata ajaira" alisema Mr Yu Viangqian.