Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na rushwa
TAKUKURU, Dk Edward Hoseah, amechaguliwa
kwa mara nyingine kuwa Rais wa Shirikisho la Mamlaka za Kuzuia na Kupambana na Rushwa Afrika Mashariki (East
African Association of Anti-Corruption Authorities- EAAACA).
Uchaguzi huo umefanyika leo Jijini Entebe – Uganda , katika Mkutano Mkuu wa nane wa
shirikisho hilo
ulioanza leo.
Katika taarifa
iliyotolewa na Afisa Uhusiano wa TAKUKURU, Doreen Kapwani inasema Dk Hoseah amechaguliwa kwa mara ya pili
kushika wadhifa huo kwani yeye ndiye aliyekuwa rais wa kwanza wa shirikisho
hilo lililoanzishwa mwaka 2007”.
Akizungumza mara baada ya kuchaguliwa kwake, Dk Hoseah
amesema katika kipindi cha uongozi wake kama
rais wa EAAACA (2015 -2017) atatoa kipaumbele
katika kuweka mikakati michache
inayotekelezeka ikiwemo kufanya tafiti za kuziba mianya ya rushwa katika mifumo
mbalimbali ya taasisi katika za nchi za Afrika Mashariki.
Pia aliongeza kuwa atamarisha uhusiano kati ya taasisi za
kuzuia na kupambana na rushwa Afrika Mashariki na kuongeza jitihada za
kuhakikisha EAAACA inajumuishwa katika Jumuiya ya Nchi za Afrika Mashariki
(East African Community).
Shirikisho hilo
linalojumuisha nchi za Tanzania ,
Kenya , Uganda , Rwanda
na Burundi , liliundwa rasmi
mwaka 2007, ambapo viongozi wa TAKUKURU (Tanzania ),
IG (Uganda ) na KACC (Kenya ) - ambao
ndio waanzilishi, walisaini Azimio la kuwa na Ushirikiano wa Mamlaka za Kuzuia
na Kupambana na Rushwa Afrika Mashariki.