“Watu wengi wamekuwa
wakiulizia kuhusu kitufe cha ‘Dislike’ (Chuki) kwa miaka mingi, na pengine
mamia ya watu wanauliza kuhusu hili. Hivyo leo ni siku ya kipekee kwani ni siku
ambayo natangaza kuwa tunalishughulikia hilo, na punde tu tutaweka kitufe hicho
kwa ajili ya majaribio.” Anaelezea Mark Zuckerberg, mmiliki wa mtandao wa
Facebook.
Zuckerberg, alieleza hayo wakati wa muda wa maswali na
majibu huko Califonia siku ya Jumanne amesema kitufe hicho hakijakusudiwa kuwa
sehemu ya kuchagua kipi ni kizuri au kibaya, au sehemu ya kupiga kura kuhusu
posti za watu.
Badala yake, amesema kitufe cha chuki kimeweka kwa ajili ya
posti ambazo zinahusisha huzuni ambapo watu hutaka kitufe cha chuki kuonyesha
kuhuzunishwa na posti badala ya kuipenda.
“Kitufe cha chuki kimewekwa kwa ajili ya kuonyesha huruma kwa marafiki,
si kwa ajili ya kuonyesha kumchukia rafiki. Wakati mwingine, rafiki huweza
kuposti kuhusu msiba wa ndugu yake, na inakuwa vigumu kupenda posti kama hiyo”. Alifafanua Mark.
Zuckerberg ameeleza kutatanishwa sana na kitufe cha chuki, na kuelezea kuwa
ndio sababu kubwa ya kucheleweshwa kwake Facebook, huku akieleza kuwa Facebook
ni sehemu ya marafiki na si sehemu ya kueneza chuki. Hivyo kitufe cha ‘Chuki”
kitafanyiwa majaribio ya mwanzo kabda ya kuruhusiwa kutumika kuwafariji
marafiki, na si kuwachukia.
Zuckerberg aliwahi kukaririwa kusema kuwa, Facebook kamwe
wasingeweza kuweka kitufe cha Chuki (Dislike), lakini kutokana na kushindwa
kujua hisia za watumiaji zaidi ya bilioni 1.5, amekuwa akiamini wote hawana
hsia za kupenda pekee.
“Kama unaelezea kitu
cha huzuni, haitakuwa kitu kizuri kupenda posti yako. Lakini marafiki zako
watahitaji kitu kukuonyesha kuwa wanaelewa hisia zako na wanakufariji.
Tuendelee kusubiri ujio wa kitufe hicho ila kwa kiasi
kikubwa kuna uwezokano wa kuja kitofauti kabisa. Kuna uwezekano wa kitufe hicho
kuja katika mfumo wa kutoa pole au kuonesha hisia za huzuni kwa kilichoandikwa
na rafiki yako badala ya kuonesha chuki n.k. Tuendelee kusubiri.