Wakazi wa Kata ya Mindu Manispaa ya Morogoro wamekumbwa na
mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu
ambapo hadi sasa mtu mmoja ameripotiwa kufa na hivyo kuzua hofu kwa
wakazi wa eneo hilo na manispaa kwa
ujumla.
Akizungumza na Mwananchi
Katika Kambi maalumu ya wagonjwa wa Kipindupindu, Afisa
Afya wa Manispaa ya Morogoro, Gabriel Malisa alimtaja aliyefariki kuwa ni Mkolole
Shomari (65).
Amesema kuwa mtu huyo alifariki nyumbani kwake maeneo ya
Mindu baada ya majirani zake ambao wametokea Dar es
salam kuwa na ugonjwa huo licha ya kuwa
walianza kutibiwa Amesema kuwa baada ya muda mfupi marehemu alianzwa na dalili za ugonjwa huo za
kuharisha na kutapika bila kuchukua
tahadhari hatimaye kupoteza maisha.
Hivyo Afisa afya huyo aliwatahazalisha wakazi wa manispaa ya
Morogoro kuwa makini na ugonjwa huo na kutoa taarifa pindi tu wanapo muona mtu
ana dalili za ugonjwa huo ili aweze kupatiwa matibabu haraka Katika eneo
husika.
Kwa upande wao baadhi ya wakazi wa kata ya mindu Abed
Ibrahim na Chales Ollynkute wamesema kuwa licha ya kuwa ugonjwa huo umeingia
Katika manispaa ya Morogoro bado wakazi wake hawana uelewa wa kutosha kuhusiana
na kujikinga na ugonjwa huo ambao umekuwa ukipoteza maisha ya watu kutokana na kutokuwa na uelewa wa kutosha.