MTENGA AMPA ONYO MCHUNGAJI MSIGWA

Bw . Hassan Mtenga Katibu wa Ccm Mkoa wa Iringa

CHAMA cha mapinduzi ( CCM) Mkoa wa Iringa kimelaani  shambulio lililofanywa na wafuasi wa chama cha Demokrasia na maendeleo ( CHADEMA) kwa wananchi waliokuwa wakitoka katika mkutano wa kampeni za mgombea Urais wa CCM Dr John Magufuli juzi.

Katibu wa CCM mkoa wa Iringa Bw.Hassan Mtenga aliwaeleza waandishi wa habari jana kuwa chama chake kinawapa pole wananchi waliopigwa na wafuasi hao wa Chadema waliotumwa na Mgombea Ubunge wa Chadema jimbo la Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa.

Mtenga alisema kuwa idadi kubwa ya waliopigwa fimbo ni wanawake kuwa tukio hilo haliungwi mkono na udhalilishaji mkubwa kwa wanawake hao

Hata hivyo alisema kuwa vitendo hivyo vya Mchungaji Msigwa kutumia vijana kupiga wananchi na wanachama wa CCM havivumiliki na kuwa iwapo Mchungaji huyo akiendelea na vitendo hivyo na kukimbia Kama ilivyokawaida yake sasa atambue wazi kuwa watamkamata na kumkapeleka polisi.

" Upole Wetu CCM ndio ambao umemfanya Mchungaji msigwa kuendelea kuwafanyia vurugu wanachama wetu ila kwa sasa tutajitolea kumkamata anaewatuma vijana hao kupiga wananchi"

Alisema hadi sasa zaidi ya wana CCM 7 katika jimbo la Iringa Mjini wamevamiwa na kupigwa na wafuasi hao wa Chadema ambao wahifadhiwa katika Gesti ya Sambala na nyingine hapa Mjini .

Akielezea kuhusu lugha za matusi anazozitoa Mchungaji Msigwa kwa Mgombea Ubunge wa CCM jimbo la Iringa Mjini Bw Frederick Mwakalebela alisema ni dalili za kuanguka kwa mchungaji Msigwa katika uchaguzi mkuu

Kwani alisema Kama angekuwa ni mbunge aliyewatumikia vema wananchi kwa kutimiza ahadi zake asingekuwa anatumia muda mwingi kutukana badala ya kueleza wananchi nini amefanya kwa miaka mitano .

Hivyo alisema kuwa iwapo Mchungaji Msigwa angekuwa na uwezo basi angesimama jukwaani kujibu zilipo Pesa za mfuko wa jimbo na kiasi cha tsh milioni 340 alizopewa na Mgombea Urais wa Chadema Edward Lowasa .

Mtenga alisema ushindi wa Mwakalebela jimbo la Iringa Mjini upo wazi kabisa na kuwa katika Mkoa wa Iringa kwa uchaguzi huu hakuna jimbo litakalokwenda upinzani.