KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi, amesema
Jeshi hilo
linamshikila aliyekuwa Mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya Chadema, Mchungaji
Peter Msigwa na wenzake 61 kwa tuhuma za kufunga barabara ya Kihesa mjini
Iringa.
Akizungumza kwenye kikao cha dharura na waandishi wa habari
kwenye kijiji cha Migori kilichopo Jimbo la Isimani mkoani Iringa, RPC Mungi
alisema Jeshi hilo
lilimtia nguvuni Msigwa na wenzake hao jana Jumatatu majira ya jioni.
Ilikuwa ni baada ya kupata taarifa kuwa watu hao walifunga
barabara ya Kihesa wakiwazuia watu waliokuwa wakienda kwenye mkutano wa kampeni
wa mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Pombe
Magufuli uliokuwa ukifanyika katika viwanja vya Samora mkoani Iringa.