PETER MSIGWA NA WENZAKE 61 WASWEKWA RUMANDE

KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi, amesema Jeshi hilo linamshikila aliyekuwa Mbunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya Chadema, Mchungaji Peter Msigwa na wenzake 61 kwa tuhuma za kufunga barabara ya Kihesa mjini Iringa.

Akizungumza kwenye kikao cha dharura na waandishi wa habari kwenye kijiji cha Migori kilichopo Jimbo la Isimani mkoani Iringa, RPC Mungi alisema Jeshi hilo lilimtia nguvuni Msigwa na wenzake hao jana Jumatatu majira ya jioni.

Ilikuwa ni baada ya kupata taarifa kuwa watu hao walifunga barabara ya Kihesa wakiwazuia watu waliokuwa wakienda kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Pombe Magufuli uliokuwa ukifanyika katika viwanja vya Samora mkoani Iringa.