Mgombea wa nafasi ya urais kupitia Chadema anayeungwa mkono
na vyama vinne vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA, Mh.Edwrad Lowassa
jana alilazimika kuahirisha mkutano
mjini Tanga baada ya maelfu ya wakazi waliojitokeza kushindwa kuenea ndani ya
uwanja wa Tangamano jijini Tanga
Kwa mara ya kwanza ndani ya jiji la Tanga shughuli zote
zinazofanyika katika mitaa ya barabara ya 4, 5,6,7, 8 zililazimika kusimama kwa muda baada ya
maelfu ya wakazi wa jiji hilo waliojitokeza katika uwanja wa Tanagmano, hali
iliyopelekea kushindwa kuendelea kwa mkutano huo kwa
sababu watu walianza
kuzimia kwa kasi