MAKAMU wa Rais, Dk. Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mhe.
Mizengo Pinda leo wameongoza mamia ya waombolezaji katika maziko ya aliyekuwa
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina Kombani
yaliyofanyika kwenye shamba lake
lililopo Lukombe nje
kidogo ya Mji wa Morogoro.
Kombani ambaye alikuwa mbunge wa Jimbo la Ulanga Mashariki
alifariki dunia Alhamisi iliyopita katika Hospitali ya Andhraprasth Appollo ya
mjini Delhi , India alikokuwa amelazwa akitibiwa
saratani ya kongosho.
Viongozi wengine walioshiriki maziko ya Mhe. Kombani ni
pamoja na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete, Spika wa Bunge Anne Makinda, Mgombea
Mwenza wa urais kupitia CCM Samia Suluhu, IGP Mstaafu Omar Mahita na wengineo.
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu Celina Kombani mahali
pema peponi. AMEN.