Rais mpya wa Nigeria Jenerali Muhammadu Buhari atahudumu pia
kama waziri wa mafuta.
Msemaji wa rais Femi Adesina amethibitisha kuwa Jenerali
Buhari ambaye katika miaka 80 alipoiongoza nchi hiyo alishikilia wadhfa wa
waziri wa mafuta atahudumu kama waziri.
Hata hivyo naibu waziri ndiye atakayechukua majukumu ya kila
siku katika wizara hiyo.
Buhari ambaye aliahidi kupambana dhidi ya rushwa na
ubadhirifu wa mali ya umma
inayotokana na mafuta amekuwa nchini Marekani katika kikao cha viongozi wa
dunia cha kongamano la umoja wa mataifa huko New York .
Uchimbaji mafuta unachangia asilimia 70% ya pato la taifa katika uchumi huo mkubwa zaidi barani Afrika hata hivyo asilimia kubwa ya pesa hizo huibiwa na kufichwa nje ya nchi.
Jenerali Buhari anatarajiwa kutangaza rasmi baraza la mawaziri wake hii leo.
Rais huyo mpya wa Nigeria alichukua hatamu za kuingoza taifa hilo yapata miezi minne iliyopita.