Huenda jitihada za Ray C kukirejesha kiuno chake kisichokuwa
na mfupa zimeanza kuzaa matunda!
Muimbaji huyo ambaye jina lake halisi
ni Rehema Chalamila, ameshare picha zake mpya kuonesha hatua aliyofikia
Kwa muda mrefu muimbaji huyo amekuwa akijaribu kuupunguza
unene wake uliompoteza muonekano wake wa zamani uliompa sifa jukwaani na sasa
picha zake mpya zinaonesha mafanikio.
“Haka ni
kanani???yaani sitaki kuamini haka katoto ni mimi uwiii !jamani nina furaha
sana moyoni kumuona ray c.wa miaka ile yaani acha tu!je nipungue zaid au?sasa
ndio muda wa kurudi rasmi kwenye muziki Babutale, Mkubwafela dada yenu niko
tayari sasa,” ameandika.