Marehemu Charles John Mallya enzi za uhai wake.
Akizungumza na gazeti hili kwa masikitiko, Philomena alisema
uchochezi mkubwa ulifanywa na watoto wa nyumba zingine ndogo (wake
wenzake).“Tangu ujana tulihangaika na marehemu na kufanikiwa kupata mali nyingi, nikiwa kama
mshauri wake lakini sasa watoto wa wake zake wengine wawili waliyokuwa katika
mikono yangu wamefikia hatua ya kunidhulumu kila kitu. Hivi sasa naishi kwenye
kijumba kidogo nilichojengewa na ndugu zangu,” alisema mwanamke huyo huku
akilia.
Philomena aliendelea kusema kuwa, hitaji lake kubwa ni
kupewa nyumba moja ya ghorofa iliyoko Sinza na nyumba ambayo haijaisha iliyoko
Moshi, Kilimanjoro.Naye mmoja wa watoto wa mama huyo, Brighton Mallya
akisimulia hali hiyo, alisema: “Baba aliacha mali nyingi na kutamka kuwa ni
aseti ambayo kila mtu akipata shida ataweza kutatuliwa kupitia mali hizo kwa
utaratibu na makubaliano, lakini sasa zimetekwa na baadhi ya ndugu.”
Kwa mujibu wa nyaraka zenye mali
za marehemu Mallya, sehemu ya mali
alizoziacha ni kampuni ilitwayo Mti Mmoja Enterprises, jina linalotumika katika
baadhi ya miradi. Pia aliacha maduka 2, mashamba, biashara ya magari, viwanja
zaidi ya 4, nyumba za kawaida, nyumba 3 za biashara ambazo ni ghorofa (zina
vyumba 105) pia kuna nyumba zingine za biashara ikiwemo Mariana Bar, Mti Mmoja
Annex na Mti Mmoja Guest ambazo ziko Sinza Mugabe, Dar.
Mwaka 1963 alimuoa Joyce Mowo na kufanikiwa kupata naye
mtoto mmoja. Mwaka 1977, Solome aliaga dunia na mwaka huohuo alimuoa Mariana
ambapo mwaka 2010, mwezi Machi, ndipo mzee huyo alikumbwa na mauti kwa maradhi
ambayo hayakutajwa.