Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho
Kikwete (pichani) amewataka wananchi wote wenye haki ya kupiga kura kuhakikisha
wanaheshimu maagizo ya Tume ya Uchaguzi ya kuwataka waondoke katika vituo vya
kupigia kura mara baada ya kumaliza zoezi la upigaji kura.
Rais Kikwete Amesema kuwa wenye jukumu la kukaa kituoni ni
Mawakala wa wagombea na sio wapiga kura wote kama
inavyodaiwa na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa.
Rais Kikwete ametoa kauli hiyo leo mjini Dodoma wakati wa kilele cha Mwenge wa Uhuru
kilchoenda sanjari na kumbukumbu ya miaka 16 ya kifo cha Baba wa Tiafa Mwalimu
Julius Kambarage Nyerere.
“Mlinzi wa uhakika wa kura ni wakala kwani ndiye anayekuwepo
wakati wote katika chumba cha kupigia na kuhesabia kura…ni jambo la kushangaza
kuona baadhi ya viongozi wa vyama vya
siasa wakiwahamasisha wafuasi wako kubaki vituo mita 100…wanalinda nini? wakati
kuna Mawakala ndani” alihoji Rais Kikwete.
Amesema kuwa ikiwa
wapiga kura wengi watabaki vituoni kwa madai ya kulinda kura upo uwezekano
mkubwa wa kutokea fujo ambazo zitasababisha baadhi ya watu kuogopa kupiga kura
na hivyo kukosa haki yao
ya msingi ya kuwachagua viongozi wanaowataka.
Rais Kikwete amesema kuwa ni vema wananchi wenye sifa za
kupiga kura kuondoka kwenye vituo mara
baada ya zoezi hilo , vinginevyo hatua kali za kisheria
zitachukuliwa kwa yoyote atakaye kaidi agizo la Tume ya Tiafa ya Uchaguzi.
Amesema kuwa watu wenye nia ya kufanya hivyo wasiilazimishe
Serikali ifikie uamuzi wa kuchukua hatua kwa kuwa wanaofanya hiyo wana nia ovu na nchi hii.
Amesesisitiza kuwa nia yao
ovu haitafanikiwa kwani Serikali imejipanga vizuri ili kuhakikisha kila
mwananchi wenye sifa ya kupiga kura anafanya hivyo bila bughuza yoyote.
Aidha , Rais Kikwete amewaonya wananchi wote wanaonunua na
kuuza vitambulisho vya kupigia kura kuacha tabia hiyo la sivyo dhidi yao
zitachukuliwa, Amesema kuwa ni vema kila mwananch akatunza vizuri kitambulisho
chake ili siku ya kupiga kura aende katika kituo cha kupigia kura ili kutekeza
haki yake ya kidemokrasia.
