SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA HUSSEIN MAFISI MBARONI,HILI NALO JIPU SUGU

Siku kadhaa nyuma niliweka Uzi unaosema Hussein Mafisi analindwa na nani?
Kwenye Uzi huo nililalamika ni nani anayemlinda Hussein Mafisi muuza madawa maarufu Mwenge. Leo muda wa saa 9 na dakika 45 amekamatwa. Gari tatu za Polisi zilifika Dukani kwake na kubeba mateja wote waliokuwepo na Hussein wenyewe..

Hii ni mara ya kwanza kukamatwa, daima hukamatwa mateja na yeye huachwa, lakini Leo kakamatwa. Nitasikitika Sana kama nitamkuta tena jioni akiendelea na biashara yake.