Jela miaka 5 kwa kuiba Mahindi ya msaada

Watumishi wawili wa halmashauri ya wilaya ya Maswa mkoani Simiyu wamefungwa jela miaka mitano kwa kosa la wizi wa mahindi ya msaada katika kijiji cha Masamwa tukio la wizi walikifanya Januari 7 na 8,2013.Mahindi hayo ni Tani 10.77 zenye thamani ya Sh 13275000.Waliokumbwa na adhabu hizo ni CHARLES KISENHA (VEO BUSHITALA) na ISACK GAMBISHI (AFISA KILIMO KATA YA BUSILILI).