Zarinah Hassan ‘Zari’.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, mama Tiffah ametakiwa kutofanya shoo kama ile kutokana na ile ya mwaka jana iliyofanyika Ukumbi wa Mlimani City, Dar kuandaliwa kwa kukiuka baadhi ya masharti.
“Jamani kwa taarifa nilizozipata kutoka Basata (Baraza la Sanaa la Taifa), zinadai kuwa, Zari kwa sasa hataruhusiwa kuandaa tamasha hapa nchini hadi pale atakapofuata kanuni za Basata.
“Inasemekana Basata wamemuwekea ngumu baada ya kuandaa tamasha lake la mwanzo huku akishindwa kufuata baadhi ya taratibu zinazostahili kabla ya kuanza maandalizi.
Ili kuisikia ishu hiyo kutoka Basata kwenyewe, juzi, Amani lilimpigia mmoja wa maafisa kutoka Basata ambapo alisema ni kweli Zari alikiuka baadhi ya taratibu ambapo alianza kutangaza shoo hiyo kabla ya kutoa taarifa Basata hivyo alipigwa fani ya shilingi laki tano (500,000).
“Kwa sasa sijui kama Zari anaweza kuruhusiwa kuandaa tamasha kwani kipindi kile anaandaa Zari All White Party alikiuka baadhi ya mambo likiwemo kuanza kutangaza shoo kabla ya kupata ruhusa kutoka Basata.
Rais Dk. John Pombe Magufuli.
Ili kusikia kutoka kwa Zari, Amani lilimpigia simu mzazi mwenzake Zari, Mbongo Fleva Nasibu Abdul ‘Diamond’ au baba Tiffah ambaye hakupokea na alipotumiwa meseji kwa simu ya mkononi, hakuijibu.