Wema Sepetu amdiss Diamond kwa namna isiyo rahisi kuijua!

Si unajua kuna lile sakata la jina Simba ambalo Diamond amekuwa akilitumia na Mr Blue hivi karibuni kudai alilianzisha yeye?

Na sasa issue hiyo inaenda mbali zaidi. Wema ametumia Instagram kuingia pia kwenye issue hiyo katika njia ambayo inaishia kuwa dongo kwa ex wake.

“Watu walikuwa wanasubiria na mimi nitaje jina langu la mnyama… Mi ni Mnyama Ndio na Jina Langu ni WEMA SEPETU…. Gnyt Y’all…. Langu mwenyewe hilo…. Ila Balozi Kasema…. hihihihihi,” aliandika Wema.

Bila shaka bado hujaiona diss! Acha tukusanue. Diss ipo kwenye mstari huu ‘Ila balozi kasema.’

Kivipi? Siku ya show ya Alikiba kwenye boxing day, hitmaker huyo alijinadi kuwa yeye ni balozi wa wanyama – akimaanisha ubalozi wake wa Wild Aid, taasisi inayopigia debe haki za wanyama.

Wengi waliistafiri kauli hiyo kama dongo kwa wote wenye majina ya wanyama!