RAIS WA MAGUFULI AMEFANYIA KAZI SUALA LA BANDARI YA DAR ES SALAAM-SYROSE BHANJI.

BUNGE la Afrika Mashariki limesema kuwa changamoto zilizokuwepo katika Bandari ya Dar es Salaam zimeweza kufanyiwa kazi na Rais Dk.John Pombe Magufuli na kufanya Bandari hiyo kutoa huduma kwa ufanisi.


Hayo ameyasema leo Mwakilishi Bunge hilo, Shy Rose Bhanji wakati Wabunge wa Afrika Mashariki Tanzania walipokutana na Spika Bunge, Job Ndugai kwa ajili ya kufahamiana kutokana wabunge hao wanatokana na bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Amesema kuwa Bunge la Afrika Mashariki lilikuwa walikuwa wakizungumzia juu ya bandari ya Dar es Salaam katika utoaji uwa huduma lakini sasa Rais Dk.John Pombe Magufuli ameweza kufanyia kazi.
Shyrose amesema wataendelea kutoa ushirikino kwa Rais katika kutumia farsa yake ya Hapa Kazi Tu katika kuwahudumia watanzania.

Nae Mwakilishi wa Spika Owen Mwandumbimbya ambaye ni Afisa Habari wa Bunge amesema kuwa Spika atatoa ushirikiano kwa wabunge kupitia kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.
  Spika wa Bunge, Job Ndugai akiwatambulisha wabunge wa bunge la Afrika Mashariki waliofika ofisini kwake leo katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam kwaajili ya kumpongeza kwa kuchaguliwa kuwa spika wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa serikali ya awamu ya tano.

 Mbunge wa bunge la Afrika Mashariki, Shy Rose Banji akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kufika katika ofisi  ndogo za bunge kwaajili ya kumpongeza Spika wa Bunge, Job Ndugai na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mbunge wa Bunge la Afrika, Shy Rose Banji jijini Dar es Salaam leo katika Ofisi ndogo za Bunge.