DAWA YA KUTIBU UGONJWA WA TETEKUWANGA (CHICKEN POX)

Tetekuwanga ni ugonjwa unasababishwa na virusi viitwavyo Varicel Zoster. Ugonjwa huu una ambukizwa kwa haraka sana. Vipele hufanana na malengelenge; na vinawasha sana. Ugonjwa huu ni wa hatari zaidi kwa watoto wachanga,watu wazima na wale ambao kinga ya mwili imeshuka.

Dalili
Vipele vya ugonjwa huu huanzia kwenye kiwiliwili na usoni kisha kuenea mwili mzima. Vipele vinafanana na lengelenge, vinawasha kisha huacha kovu. Makovu ya ugonjwa huu si ya kudumu kwani baada ya muda hufifia.

Dalili nyingine ambazo hujitokeza siku moja au mbili kabla ya vipele ni

  1. -homa kali
  2. -uchovu
  3. -kukosa hamu ya kula
  4. -maumivu ya kichwa


Maambukizi

  • Ugonjwa huu husambaa kwa njia ya hewa pale mgonjwa anapopiga chafya au kupenga. 
  • Pia huweza kusambaa endapo endapo utakugasana na majimaji yenye virusi toka kwa mgonjwa. Mgonjwa huanza kuambukiza kabla vipele havijatoka na huendelea kuambukiza mpaka makovu yanapotoka.
  • Ukiugua ugonjwa huu mara moja unaweza kupata kinga ya kudumu. Mtu aliyewahi kuugua tetekuwanga anaweza kuugua mkanda wa jeshi.


Kinga.
Unaweza kujikinga na ugonjwa huu iwapo utapata chanjo. Katika nchi zilizoendelea chanjo za ugonjwa huu hutolewa kwa watoto wote.

Matibabu

  • Kwa kawaida ugonjwa huu hauitaji dawa lakini kama dawa ikianzishwa ndani ya masaa 24 huleta manufaa na hupunguza dalili za ugonjwa kwa kiasi kikubwa. 
  • Matibabu makubwa hulenga kudhibiti dalili kam homa, mwili kuwasha na upungufu wa maji mwilini.


Hata hivyo watu wenye upungufu wa kinga, wanaotumia dawa za kushusha kinga, saratani ya ngozi, wajawazito wanahitaji uangalizi maalumu.

TETEKUWANGA:

  • Ugonjwa wa tetekuwanga husababishwa na vijidudu vidogo sana aina ya vijasumu. huanza wiki 2 hadi 3 baada ya mtoto kukaa na mtoto mwingine ambaye tayari anao ugonjwa huu.
  • Kwanza kabisa, madoadoa au vipele vidogo sana vyekundu na ambavyo huwasha, huanza kutokea.
  • Hivi, hubadilika na kuwa malengelenge na mwishowe, kufanya ganga vyote kwa wakati mmoja.
  • Kawaida huanza kwenye mwili na baadaye hutokea kwenye uso, mikono na miguu.
  • Kunaweza kukawa na vipele, malengelenge, na ganga vyote kwa wakati mmoja. Kwa kawaida homa ni kidogo tu.


Tiba:
Ugonjwa hupona baada ya wiki moja. Ukoge kila siku kwa sabuni na maji ya uvuguvugu ili kupunguza kuwasha. Tumia nguo baridi zilizoloweshwa kwenye maji yaliyotokana na shayiri iliyochemshwa na kukamuliwa.
Kata kucha za mikono ziwe fupi kabisa. Kama ganga zinapata ugonjwa, paka gentia violet (g.v) au mafuta ya kuua vijidudu.

Utatuzi wa kiasili wa tetekuwanga ni pamoja na maji ya pea, magadi ya kuoka , mafuta ya vitamini E , asali, chai mitishamba au karoti na korianda. Inaaminika kwamba muwasho wa ngozi unaweza kupunguzwa kwa

kiwango fulani kwa maji ambayo yametumika kupikia mbaazi mabichi. Losheni inayotengenezwa kwa magadi ya kuoka na maji yanaweza kuwekwa kwenye ngozi za wagonjwa kwa sponji ili kupunguza mwasho. Pia, kupaka

mafuta ya vitamini E au asali kwa ngozi hudhaniwa kuwa na athari ya uponyaji kwa alama ambazo zinaweza kubakia baada ya maambukizi kutibiwa. Baadhi ya watu wanadai kuwa athari za kutuliza kwa kadri za chai ya kijani zina ufanisi wa kupunguza dalili.