Mbegu ndio msingi wa kiumbe hai chochote. Mbegu za mazao kama mpunga hutunza sifa za kijenetiki za mmea hivyo matumizi ya pembejeo zingine za kilimo ni katika tu kusaidia mbegu iweze kutoa mavuno kwa kiwango kinachotegemewa. Ndio maana pembejeo zingine kama mbolea zisipotumika mbegu huweza kutoa mavuno kidogo tu lakini pembejeo zingine hizi haziwezi kutumika bila mbegu.
1. Umuhimu na kanuni za mbegu bora.
a. Kwanini mbegu bora?
Mbegu bora za mpunga zimetafitiwa ili kukidhi mahitaji ya wadau muhimu katika sekta ya mpunga kama vile:
i. Wakulima --- Mavuno mengi
ii. Wasindikaji --- Ukobolekaji
iii. Wafanyabiashara --- Mwonekano k.m. punje ndefu na nyembamba
iv. Walaji --- Radha, kupikika,
b. Faida za kutumia mbegu bora
Mfano:
1. Umuhimu na kanuni za mbegu bora.
a. Kwanini mbegu bora?
Mbegu bora za mpunga zimetafitiwa ili kukidhi mahitaji ya wadau muhimu katika sekta ya mpunga kama vile:
i. Wakulima --- Mavuno mengi
ii. Wasindikaji --- Ukobolekaji
iii. Wafanyabiashara --- Mwonekano k.m. punje ndefu na nyembamba
iv. Walaji --- Radha, kupikika,
b. Faida za kutumia mbegu bora
- Zimetiwa dawa ya kuzuia magojwa ya udongoni, vijidudu na fangasi hivyo kuiepusha mbegu na mche kutokana na mashambulio ya magonjwa, wadudu na fangasi.
- Zina uotaji wa kiwango cha juu hivyo huokoa gharama ya mbegu. TOSCI hudhibitisha mbegu ya mpunga ikiwa tu uotaji wake ni zaidi ya 80%.
- Huokoa gharama
Mfano:
Jedwali la matumizi ya mbegu katika Ekari moja na gharama zake
Mbegu
|
Kiasi cha mbegu kwa Ekari
|
Gharama ya mbegu
|
Jumla ya gharama ya mbegu
|
Mbegu bora iliyothibitishwa
|
Kilo 4 hadi 8
|
TSH 3,000 kwa kilo
|
12,000 hadi 24,000
|
Mbegu isiyo bora
|
Debe 2 hadi 3
|
TSH 10,000 kwa debe
|
20,000 hadi 30,000
|
c. Mbegu bora
- Ni halisi (genetic pure)
- Ni safi, haina mchanga, mapepe wala masuke
- Viwango vya uotaji viko juu
- Hutoa mimea yenye afya njema
- Huvumilia baadhi ya magonjwa na wadudu
- Hukomaa pamoja
- Mchele wake huiva kwa pamoja ukipikwa
2. Uzalishaji wa mbegu bora
a. Uchaguzi wa shamba na maandalizi kwa ajili ya uzalishaji wa mbegu
Sifa za shamba
i. Tambarare, lisilo na miinuko
ii. Lisilo na mafuriko
iii. Lisilo na vivuli
iv. Kuingiza maji na kuyatoa kiurahisi (good drainage)
b. Kukokotoa Kiasi cha mbegu
Kiasi cha mbegu = mbegu inayotakiwa kwa ekari x eneo (ekari)
Uotaji (%)
c. Utenganisho wa shamba la mbegu ya na mashamba mengine ya mpunga
Uchavushaji waweza kusababishwa na:
- Upepo
- Wadudu
- Ndege
- Konokono
- Maji
Shamba la mbegu ya mpunga iliyothibitishwa litengane na mengine kwa mita
d.Uthibiti magugu
- Magugu hupunguza wingi na ubora wa mbegu
- Shamba liwe safi muda wote
- Sheria mbegu imekataza aina fulani ya magugu kutokuwepo kabisa shambani k.m bhangi, mpunga pori, kiduha
e.Kuondoa mimea isoyo mbegu (off-type)
Mfano wa off-type
- Mimea ya mpunga iliyojiotea yenyewe mathalan kutoka msimu uliopita
- Kubadilika kwa sifa za kijenetiki za mmea
- Mchanganyiko wa mbegu kwa bahati mbaya
- Utambuzi wa off-type
- Mimea mifupi ama mirefu zaidi ya wenzao shambani
- Mimea yenye rangi tofauti za majani, masuke
- Mkia wa punje (awn)
- Mimea inayowahi zaidi ama kuchelewa zaidi kuchanua (mimea itofautiane kati ya siku 2-3)
- Mkao wa jani la juu katika suke (lag leaf angle)
- Ukubwa, umbo na rangi ya punje
- Mimea iliyoshambuliwa na ugonjwa/wadudu
- Kuondoa maotea (off-type) kufanyike angalau mara moja wakati wa:
- hatua ya ukuaji wa majani (vegetative growth)
- kuchanua
- baada ya kuchanua
- kabla ya kuvuna
f. Udhibiti wa wadudu na magonjwa shambani
Ifahamike kwamba, wadudu na magonjwa huathiri wingi na ubora wa mbegu ya mpunga hasa viwapo shambani.
g. Matumizi ya mbolea
Matumizi sahihi ya mbolea huongeza ubora na wingi wa mavuno ya mbegu ya mpunga.
3. Uvunaji na huduma baada ya kuvuna mbegu bora
a. Muda wa kuvuna (Timing)
Kuwahi ama kuchelewa hupunguza ubora na mavuno
Athari ya Kuwahi kuvuna
- Mbegu zisizojaza vizuri
- Mavuno/ubora kidogo
- Kupoteza uotaji
- Athari za Kuchelewa kuvuna
- Mashambulizi ya wadudu, ndege
- Kuanguka
- Kupukutika
- Muda sahihi wa kuvuna
- Punje hugeuka kuwa njano-kahawia
- 80% ya majani imebadili rangi kutoka kijani na kuwa rangi ya mabua
- Unyevu wa punje 20-22%
- Punje huwa ngumu na hazivunjiki kirahisi zikitafunwa
b. Kukausha mbegu ya mpunga
Mbegu yenye unyevu kidogo huweza kutunzwa kwa kipindi kirefu bila kuharibika (kuvuna, kupoteza uotaji).
Unyevu wa mbegu
|
Muda wa kudumu gharani
|
14-18%
|
Wiki 2 -3 tu
|
13%
|
Miezi 8-12
|
9%
|
Zaidi ya mwaka
|
4. Viwango vya mbegu
Mbegu bora huzalishwa kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu hivyo vimewekwa viwango ambavyo ili mbegu ithibithishwe ni lazima vifikiwe.
Vipo viwango vya shambani na maabara kama ifuatavyo:
a. Viwango vya shambani
Kigezo
|
Kiwango
|
Shamba (misimu kabla)
|
2
|
Utenganisho
|
mita 5 na zaidi
|
Awamu za ukaguzi
|
2 na zaidi
|
Maotea (off-types)
|
0.1
|
Mazao mengine
|
0.05%
|
Magugu yaliyozuiwa
|
0
|
Mimea ya Mpunga pori
|
0.1%
|
b. Viwango vya maabara
Kigezo
|
Kiwango
|
Mbegu halisi (Pure Seed)
|
98.0% na zaidi
|
Mbegu zingine (Other Seed)
|
0.1 na pungufu
|
Makapi (masuke, vijiti, majani)
|
1.9% na pungufu
|
Unyevu wa mbegu
|
13.0% na pungufu
|
Uotaji
|
80% na zaidi
|
Mbegu za magugu yaliyozuiliwa
|
0.0%
|
Mbegu za magugu yayokatazwa
|
punje 4 kwa kilo na pungufu
|
Baadhi ya Magugu yaliyozuiliwa
- Kiduha/Magugu chawi (sani)
- Bangi
- Kokeini
Magugu yaliyokatazwa
- Ndago
- Mpungapori
- Mashikanguo