Waziri Mhagama pia amepiga marufuku kwa watumishi wa Hospitali zote kutowauzia dawa za Methadone waathirika wa dawa za kulevya kwakuwa ilishatangaza kuwa ni bure…>>’Tumetoa onyo kali, na kila mtoa huduma ambaye atakiuka misingi ya huduma hii atachukuliwa hatua‘
Kama wewe ni mtumiaji wa Shisha hii pia inakuhusu, Waziri Mhagama anasema..>>>’Tumeanza kufanya utafiti na tumegundua kwamba kuna kila dalili ya matumizi ya dawa za kulevya katika shisha‘
‘Niwaombe Watanzania haswa vijana wanaojihusisha katika matumizi ya shisha katika maeneo ya starehe wachukue tahadhari sana, ni eneo ambalo linapelekea matumizi ya dawa za kulevya‘