YANGA MBELE KWA MBELE

Yanga imeendelea kushinda mechi zake za ligi kuu Tanzania bara baada ya kuifunga Toto Africans ya jijini Mwanza kwa magoli 2-1 kwenye uwanja wa CMM Kirumba, Mwanza.

Toto walianza kupata goli la kwenye mchezo huo lililofungwa na William Kimanzi dakika ya 39 kipindi cha kwanza lakini goli hilo likasawazishwa na Amis Tambwe dakika ya 50 kipindi cha pili.

Yanga walijihakikishia pointi tatu kwenye mchezo huo kupitia beki wao wa kulia Juma Abdul dakika ya 78 na kifanya Yanga kufikisha pointi 65 baada ya kucheza michezo 26 ya VPL.