Waombaji ajira kwa mtandao waongezeka

Dar es Salaam. Sekretarieti ya Ajira ya Utumishi wa Umma, imesema tangu kuanzishwa kwa mfumo wa utumaji maombi kwa elekroniki umesaidia kupungua muda wa mchakato wa utumaji maombi kutoka siku 90 hadi 52.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Utumishi wa Umma, Riziki Abraham amesema mfumo wa uwasilishaji maombi.

“Uombaji umeongezeka na hivi sasa waombaji 97,765 wamejiandikisha katika mfumo huu, 89,484 wametuma maombi yao,” amesema Abraham.

Kaimu Naibu Katibu wa Tehama, Mtage Ugullum amesema mfumo huo upo chini ya wataalamu ambao watahakikisha taarifa zote zinawafikia walengwa.