Simba imempata kocha wa zamani wa Azam FC


Klabu ya wekundu wa Msimbazi Simba leo June 30 imetangaza rasmi kupitia kurasa zake za mitrandao ya kijamii kuingia mkataba na kocha raia wa Cameroon Joseph Omog, Simba wametangaza kuingia mkataba na Omog bila kuweka wazi mambo kadhaa kwa kigezo kuwa taarifa rasmi itatoka kesho July 1.

Simba wameingia mkataba na Omog ambaye amewahi kuifundisha klabu ya Azam FC na kuipatia Ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania bara msimu wa 2013/2014 kwa mara ya kwanza, Omog kwa sasa ana umri wa miaka 44 na anatajwa kuwa kesho ndio atatambulishwa rasmi kujiunga na Simba.