Drake ampa makavu Meek Mill, tena

Series ya bifu la Drake na Meek Mill bado linaendelea baada ya mapumziko mafupi kwa sababu Drake amemchana tena Meek Mill kwenye ziara yake ya ‘Summer Sixteen’.

Kwenye show hiyo iliyofanyika mjini Washington, D.C wikiendi hii Drake alitumia neno ‘Pussy’ kumtaja Meek Mill kwenye wimbo wake wa ‘Back To Back’ ambapo kwenye wimbo huo alioandika kwa ajili ya kumdiss msanii huyo neno hilo hakulitaja, “I did another. I did another one / That pussy still ain’t did shit about the other one.”

Meek Mill ndio alikuwa wa kwanza kuanzisha bifu hilo la kutupiana maneno na Drake baada ya kurap mashairi yaliyomlenga msanii mwenzake huyo. “When I see an L, that’s what I think about the most. I learned a lot from watching these ni**as that I did a lot for in this industry. I used to always hear people say, ‘This industry’s fake. These ni**as is fake.’ I tried to come in with the real ni**a approach to try to change them, but it’s too many against one,” alirap Meek.

Hata hivyo Drake yupo kwenye wakati mgumu baada ya kuwa na bifu na msanii mwengine, Joe Budden.