Facebook yawapatia wateja fursa ya kutoa tahadhari

Mtandao wa facebook umewapatia fursa wateja wake kutoa ishara ya tahadhari ya kiusalama iwapo watajipata katika hali hatari.

Kufikia sasa huduma hiyo ilikuwa inaweza kutolewa na wafanyikazi wa kampuni hiyo pekee.

Huduma hiyo ya usalama inawapatia watumiaji wa mtandao huo fursa ya kutoa ujumbe kwa marafiki ama familia zao kwamba wako salama kunapotokea janga la kibinaadamu mahala walipo.

Tetemeko la ardhi la hivi majuzi nchini Itali liliadhimisha mara 25 mwaka huu kwamba lilisababishwa.

Ujumbe huo wa usalama umewafikia watu bilioni moja mwaka 2016 pekee,kampuni hiyo imesema.
Katika kipindi cha miaka 2 iliopita kwa pamoja huduma hiyo ikutumika mara 11 pekee.

Timu ya facebook inayotoa huduma hiyo hutumia vigezo vitatu kubaini kuamua iwapo huduma hiyo inapaswa kutolewa:
Idadi ya watu walioathirika

Athari ya janga hilo

Na wakati wa tukio