Jack Wilshere kujiunga na Bournemouth

Kiungo wa kati wa Arsenal Jack Wilshere anakaribia kujiunga na klabu ya Bournemouth kwa mkopo wa muda wa msimu uliosalia baada ya mpango wa kuijiunga na klabu ya Roma kuzuiwa na Arsenal.

The Gunners ilikataa kufanya biashara na Roma kwa sababu ya vile walivyochukulia uhamisho wa beki Kostas Manolas mapema msimu huu.

Wilshere mwenye umri wa miaka 24 alifanya mazungumzo na Bournemouth na Crystal Palace.

Anatarajiwa kufanyiwa ukaguzi wa kimatibabu na The Cherries.