Virginia, Marekani
Mashuhuda wa tukio hilo waliokuwa wakisafii kwa treni wamesema walianza kuona moshi na baadaye moto ukiwaka na waliposogea eneo la tukio waliona ndege ndogo ikiwa imeanguka juu ya mti huku ikiteketea kwa moto. Aidha tarifa zimeeleza pia kuwa hakuna mtu aliyeokolewa hata mmoja, wote waliokuwemo wamefariki dunia.
Polisi katika Jimbo la Virginia wamesema watu wote waliokufa siyo raia wa Marekani na kwamba miili ya marehemu hao itapelekwa kwa Daktari Mkuu wa jimbo hilo, Richmond kwa uchunguzi ili kuwatambua na kubaini ndugu zao.